SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: NDANDA HAIKUTAKA KUVUNJA REKODI YAO KWA YANGA.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
KLABU ya Yanga imeendelea kunyimwa pointi katika uwanja wa Nangwanda Sijaona uliopo Mjini Mtwara baada ya hapo jana kulazimishwa sa...
Mshambuliaji wa Yanga Obrey amecheza kwa mara ya kwanza mechi ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara wakati Yanga ikicheza dhidi ya Ndanda FC kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara




KLABU ya Yanga imeendelea kunyimwa pointi katika uwanja wa Nangwanda Sijaona uliopo Mjini Mtwara baada ya hapo jana kulazimishwa sare tasa ya bila kufungana dhidi ya trimu ya Ndanda FC.

Katika mechi tano walizokutana kati ya klabu ya Yanga na Ndanda, sare zimezidi kutawala ambapo kuna sare 3 huku Yanga wakishinda mchezo 1 kama walivyofanya Ndanda katika mchezo wa kwanza wa timu hizi tangu Ndanda apande daraja.

Ndanda ikiwa inacheza mchezo wake wa kwanza kwenye uwanja wa nyumbani iliweza kuhimili mashambulizi ya Yanga ambayo pia ilikuwa ikicheza mchezo wake wa kwanza ugenini tangu kuanza kwa ligi msimu wa 2016-2017.

Licha ya kufanya mashambulizi ya mara kwa mara, wachezaji wa Yanga walishindwa kupata goli na kujikuta wakipata kona nyingi kutokana na walinzi wa Ndanda kuokoa mashambulizi ya hatari yaliyofanywa na Yanga.



 

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top