
SHIRIKISHO la
Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), limesambaza waraka mpya kwa wanachama wake,
likiwamo Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ukisema mameneja wote wa
usajili wa wachezaji kwa mfumo wa Mtandao (TMS-Transfer Matching System Managers)
hawana budi kujiunga na mawasiliano mapya ili kupata taarifa mbalimbali za
usajili na uhamisho wa wachezaji.
FIFA limeleta mfumo huo unaoitwa GPX
yaani Global Players Exchange ambao malengo yake ni kurahisisha kufanya usajili
kwa mchezaji mmoja kwenda timu nyingine lakini kabla ya kufanya hivyo utasaidia
kupata taarifa kamili za mchezaji huyo na shabaha kuu ni kurahisisha
mawasiliano ya TMS Managers nchi nzima, klabu na mashirikisho mbalimbali
duniani.
Hiyo inakuja baada ya baadhi ya
mashirikisho kama vile TFF kuwa na matatizo lukuki ifikapo kipindi cha usajili
na hivyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matatizo yafananayo na hayo.
Post a Comment