Kikosi bora cha Euro 2016.
Ronaldo aliwahi kujumuishwa katika kikosi cha
mashindano ya ulaya mwaka 2004 akiwa na umri wa miaka 19 lakini pia na mwaka
2012.
Raia mwenzake, Pepe pia yupo kwenye kikosi hicho na
aliwahi pia kujumuishwa 2008 na 2012.
Awali, kulikuwa
kukitajwa kikosi cha wachezaji 23 lakini wakati huu kimetajwa kikosi cha wachezaji
11
Kikosi kamili
kinajumuisha (4-2-3-1): Rui Patrício (Ureno); Joshua Kimmich (Ujerumani),
Jérôme Boateng (Ujerumani), Pepe (Ureno), Raphaël Guerreiro (Ureno); Toni Kroos
(Ujerumani), Joe Allen (Wales); Antoine Griezmann (Ufaransa), Aaron Ramsey (Wales),
Dimitri Payet (Ufaransa); Cristiano Ronaldo (Ureno).
Kikosi hicho kiliteuliwa na jopo la kiufundi cha
Uefa lililojumuisha, miongoni mwa wengine, Sir Alex Ferguson na David Moyes.
“Tunaamini kikosi hiki cha wachezaji 11
kinawakilisha wachezaji bora zaidi walioshiriki michuano,” amesema, Ferguson,
ambaye ni balozi mwema wa ukufunzi wa Uefa.
Post a Comment