SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: West Ham: Yamnasa Gokhan Tore Kutoka klabu ya Besiktas kwa Mkopo.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
West Ham: Yamnasa Gokhan Tore Kutoka klabu ya Besiktas kwa Mkopo. West Ham wamefanikiwa kumsajili winga machachari kutoka klabu y...

West Ham: Yamnasa Gokhan Tore Kutoka klabu ya Besiktas kwa Mkopo.

Gokhan Tore



West Ham wamefanikiwa kumsajili winga machachari kutoka klabu ya Besiktas kwa mkopo, akitia kandarasi ya mwaka mmoja huku kukiwa na uhuru wa kumsajili jumla endapo atakuwa na msimu bora klabuni hapo.

Tore raia wa Ujerumani aliyezaliwa nchini Uturuki, ameichezea timu ya vijana ya Chelsea kwa miaka miwili kabla ya kuihama klabu hiyo na kusajiliwa na Besiktas

Tore aliisaidia klabu yake kuichapa klabu ya Fenerbahce na kuchukua ligi ya Uturuki.

Tore mwenye umri wa miaka 24 amesema, Bilic alikuwa ni sababu ya yeye kuhama uwanja wa Olympic na kuongeza kuwa alikuwa ni meneja bora kwa wakati wote nikiwa naye.


Tole alishinda magoli manne na Kutoa pasi za magoli sita katika michezo 24 aliyocheza akiwa na Besiktas wakishinda kombe la ligi kwa tofauti  ya point 5

‘‘Bilic ni mtu muhimu sana kwangu na ananifahamu vizuri sana, nisingeweza kusema hapana kwake”  Alisema Tore.

‘‘Ni kama baba kwa wachezaji, unajihisi kama ni familia”  alieleza Tore.

Uongozi wa West Ham umesema, Tore atajiandaa kwa msimu ujao akiwa katika  uwanja wa mazoezi wa timu wakati wachezaji wengine wa kikosi cha kwanza wakiwa katika Tour yao huko Marekani.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top