Mshambuliaji wa Southampton
Graziano Pelle: ajiunga na timu
ya Shandong Luneng ya Nchini China.

Mshambuliaji wa kimataifa wa iItalia aliyekuwa akikipiga katika
klabu ya Southampton ya nchini Uingereza, amejiunga na klabu ya Shandong Luneng
inayoshiriki super league ya nchini
China kwa uhamisho wa paund 12m.
Pelle mwenye umri wa miaka 30, alijiunga na ligi ya EPL msimu wa
2014 akitokea katika klabu ya Feyenoord ya nchini Uholanzi na kuishindia Sants magoli 30 katika mechi 81
alizocheza Pelle.
Pelle aliitwa katika kikosi cha timu ya taifa akiwa anaichezea
klabu ya Southampton na alikuwa sehemu ya kikosi kilichoshiriki katika
mashindano ya EURO yaliyomalizika hapo siku ya jana na kuifungia timu yake ya
taifa magoli mawili.
Pelle anakuwa mchezaji wa tatu kuihama klabu ya Southampton baada
ya kushuhudia raia wa Kenya Victor Wanyama kusajiliwa na klanu ya Tottenham
lakini pia Sadio Mane akijiunga na majogoo wa anfield, klabu ya Liverpool.

Pelle aliyewahi kuzichezea klabu za Parma pamoja na AZ Alkmaar, amejiunga na aliyowahi kuwa
mchezaji wa zamani wa New castle Papiss Cisse ambao kwa sasa wako chini ya kocha aliyewahi
kuifundisha klabu ya Fulham ya nchini Wingereza Felix Magath.
Klabu ya Southampton wanakaribia kuinasa saini
ya mchezaji kiungo mkabaji wa Bayern Munich Pierre-Emile Hojbjerg ambaye
anafanyiwa vipimo vya afya kabla ya kutangazwa rasmi kwa kitita cha paund 12.8m.
Post a Comment