
Mshindi mara mbili wa mashindano ya Australian Open Victoria Azarenka
amefichua kwamba ana mimba.
Raia huyo wa Belarus mwenye umri wa miaka 26 amesema anapanga
kurejea katika uchezaji baada ya kujifungua mwishoni mwa mwaka huu.
Azarenka na mpenzi wake waligundua kwamba alikuwa mjamzito
alipokuwa anauguza jeraha la goti.
"Tuna furaha sana na najihisi kubarikiwa kwamba nitaanza
safari hii ya kusisimua,” amesema Azarenka, ambaye ameorodheshwa nambari sita
kwa ubora duniani.
"Nimetiwa moyo sana na wanamichezo wengine wa kike ambao
huweza kurejea kushindana baada ya kujifungua na ninapanga kufanya vivyo
hivyo.”
Azarenka
alishinda Australian Open mwaka 2012 na 2013, miaka ambayo pia alifika fainali
US Open lakini akashindwa.
Hajacheza tangu
aondoke uwanjani raundi ya kwanza mechi ya French Open dhidi ya Mwitaliano
Karin Knapp mwezi Mei.

Huo ulikuwa ni waraka wa Victoria Azarenka akiwaandikia mashabiki wake na kuweza kuupost kwenye akaunti yake rasmi ya twitter.
Post a Comment