SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SIMBA, AZAM KUKUTANA FAINALI MAPINDUZI CUP.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
NI jambo jepesi sana kuiendeleza rekodi kuliko kuivunja na hicho ndicho Simba walichokifanya baada ya kuwagaraza klabu ya Yanga na k...
dsc_0291


NI jambo jepesi sana kuiendeleza rekodi kuliko kuivunja na hicho ndicho Simba walichokifanya baada ya kuwagaraza klabu ya Yanga na kuwaachia kidonda baada ya kuwaondosha kwenye mapinduzi Cup kwa jumla ya penalt 4-2.

Mchezo huo ulioshuhudia timu hizo zikitoshana nguvu kwa dakika zote 90, ambapo mwamuzi wa mchezo huo aliamuru kupigwa matuta yaliyopeleka maumivu mitaa ya Jangwani.

Penati za simba zilipigwa na Jonas Mkude, Daniel Agyei, Mzamiru Yassin na Javier Boukungu huku Method Mwanjale akiwa ni mchezaji pekee wa Simba aliyekosa penati ambayo iliokolewa na golikipa wa Yanga Deogratius Munishi.
Simon Msuva na Thaban Kamusoko ndio wachezaji pekee wa Yanga waliofunga penati zao huku Deogratius Minish ‘Dida’ na Mwinyi Haji penati zao zilitua kwenye mikono ya golikipa wa Simba Daniel Agyei.
Mashindano hayo yanatarajia kufikia tamati siku ya Ijumaa ambapo maadhimisho ya siku yenyewe ya Mapinduzi ni siku ya Alhamisi.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top