
KOCHA
wa timu ya West Ham, Slaven Bilic amethibitisha ya kuwa mshambuliaji wao
tegemezi, Dimitri Payet amegoma kusaini mkata wa kuendelea kubaki klabuni hapo.
Kufuatia taarifa hiyo,
Bilic ameamua kumtoa kwenye kikosi kitakachocheza na Crystal Palace siku ya
jumamosi.
Payet alikuwa na msimu
bora sana uliopita na kuisaidia timu kupata matokeo chanya hivyo anataka
kuondoka klabuni hapo ili akatafute maisha sehemu nyingine.
“Ndio hili lipo kwamba
Payet anataka kuondoka, hataki kufanya mazoezi na timu na tulishasema
hatutawauza wachezaji wetu bora kama Payet” Alisema Bilic.
Mabingwa wa ligi ua
Ufaransa, klabu ya PSG wanahusishwa kutaka kumsajili Payet raia wa Ufaransa
ambaye ameshapachika mabao 15 ndani ya mechi 60 alizocheza.
Post a Comment