
KUFUKUZWA kwa aliyekuwa kocha wa klabu ya
Chelsea, Jose Mourinho, kama mkufunzi wa Chelsea, kumeiingizia klabu gharama ya
£8.3m ikiwa ni kama fidia.
Mourinho, ambaye ni kocha wa Manchester United, alitimuliwa mwezi
December ya mwaka 2015 kufuatia matokeo mabuvu ya kushindwa kulitetea kombe la
ligi.
Chelsea, walimaliza msimu wakiwa nafasi ya 10 ya msimamo wa
EPL na taarifa ya mapato ya mwaka 2015-2016 inaonyesha klabu ilipata hasara ya Zaidi
ya £70.6m ikijumuishwa na £67m iliyolipwa kwenye kampuni ya Adidas kusitisha
mkataba.
Hata hivyo, mkataba
wa Adidas ulivunjwa ili kuingia kandarasi na kampuni ya Nike kwa Zaidi ya miaka
15 ambapo wataweza kutengeneza faida ya £30m kwa mwaka.
Mkataba wa Adidas na Chelsea ambao ulikatishwa ndani ya
miaka 6 ulikuwa umesainiwa kwa jumla ya miaka 10 ambapo ungeiingizia Chelsea
kiasi cha £30m kwa mwaka.
Post a Comment