
TIMU ya wanawake ya Nigeria imesitisha
mgomo wao wa kukaa hotelini baada ya kulipwa stahiki zao walizokuwa
wameahidiwa.
Timu
hiyo ilikuwa inalidai shirikisho la mpira la nchi hiyo NFF kiasi cha US$23,650 kwa kila mchezaji baada ya kutwaa ubingwa wa
timu za wanawake kwa bara la Africa.
Wadada hao wanaojulikana
kwa jina la The Super Falcon, wamekuwa hotelini katikati ya jiji la Abuja tangu
tarehe 6 ya mwezi December yam waka huu.
"Wachezaji
wameshaondoka wote hapa hotelini baada ya kupokea stahiki zao walizokuwa
wameahidia na NFF” Ofisa habari wa timu hiyo Remi Sulola alikiambia kituo cha
bbc.
Moja ya wachezaji hao
pamoja na mwenzake wa chumba walichokuwepo wamethibitisha kupokea fedha hizo.
"Inaweza ikachukua
muda hivi kwa sababu mabenki mengi hayafanyi kazi siku za wikiendi, lakini
hatimaye tumekwisha pokea kilicho chetu” Alisisitiza dada mmoja ambaye hata
hivyo aliomba kuhifadhiwa jina lake.
"Tunaishukuru
serikali, mashabiki pamoja na vyombo vya habari ambao mlitusaidia kuhakikisha
tunapata haki zetu”
Post a Comment