
TIMU
ya Ndanda FC ya mjini Mtwara imeendeleza uteja mbele ya timu ya Simba baada ya
kukubali kichapo cha goli 2-0 kwenye mchezo uliofanyika katika dimba la
Nangwanda Sijaona, mjini Mtwara.
Alikuwa ni Mzamiru
Yassini na Mohamed Ibrahim, MO waliopachika mabao hayo na kuirejesha Simba
kileleni kwa jummla ya pointi 38 huku wakiwaacha mahasimu wao kwa wao Yanga kwa
pointi mbili baada ya kukaa kileleni kwa muda.
Tangu klabu ya Ndanda
ipande daraja msimu wa mwaka 2014, haijawahi kupata matokeo yoyote chanya mbele
ya wekundu wa msimabazi Simba.
Takwimu
Simba vs Ndanda tangu mwaka 2014.
18/12/2016 Ndanda FC 0-2 Simba
20/08/2016 Simba 3-1 Ndanda FC
10/03/2016 Simba 3-0 Ndanda FC
01/01/2016 Ndanda FC 0-1 Simba
25/04/2015 Simba 3-0 Ndanda FC
17 01/2015 Ndanda FC 0-2 Simba.
Matokeo mengine ni:
Mbao FC 1-0
Stand United
African Lyon 0-0 Azam FC
Tanzania Prisons 1-0 Majimaji FC
Post a Comment