SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: AFFUL: ENEO LA USHAMBULIAJI LA AZAM LITAKUWA TISHIO.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
BAADA ya mshambuliaji wa kimataifa wa klabu ya Azam kuafikiana na timu hiyo, mshambuliaji huyo raia wa Ghana, Samuel Afful, ame...





BAADA ya mshambuliaji wa kimataifa wa klabu ya Azam kuafikiana na timu hiyo, mshambuliaji huyo raia wa Ghana, Samuel Afful, ameanza kupiga mkwara ya kuwa timu yao itakuwa bora msimu ujao kutokana na watu waliosajiliwa kwenye timu hiyo.

Afful, aliyetokea klabu ya Sekondi Hasaacas ya huko Ghana, amejitia kitanzi cha miaka mitatu cha kuitumikia klabu hiyo huku akiungana na wenzake Waghana waliosajiliwa na Azam FC msimu huu, beki wa kati Daniel Amoah, winga Daniel Atta Agyei na mshambuliaji Yahaya Mohammed.

Uwezo wake ulianza kuonekana pale alipofunga goli moja katika mechi ya kirafiki dhidi ya Ruvu Shootimg, pale Azam walipoibuka na ushindi wa goli 3-1.

Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu ya Azam FC www.azamfc.co.tz Afful amesema kwa aina ya wachezaji waliosajiliwa tokea Ghana akiwemo na yeye, basi ni dhahiri kuwa Azam itakuwa na safu bora ya ushambuliaji.

“Nimefurahishwa sana kujiunga na Azam FC kama mchezaji mwingine anavyofurahia kusaini mkataba mpya, namshukurtu Mungu kwani yeye ndiye aliyefanikisha hili, nimejiandaa vilivyo kuisaidia timu hii na naamini kwa namna nilivyowaona wachezaji kwenye mechi mbili walizocheza na usajili uliofanywa Azam FC itakuwa moto kwa mechi zinazokuja na eneo la ushambuliaji litakuwa tishio” Alisema Afful,

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top