SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: MAYANJA: TUNASONGA MBELE HATUANGALII NYUMA.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
KOCHA msaidizi wa timu ya Simba, Jackson Mayanja amesema wao wanachoangalia ni kusonga mbele ili kutimiza adhma yao ya kumaliza ligi r...
Mayanja J

KOCHA msaidizi wa timu ya Simba, Jackson Mayanja amesema wao wanachoangalia ni kusonga mbele ili kutimiza adhma yao ya kumaliza ligi raundi ya kwanza wakiwa kifua mbele ili kurejesha furaha kwa mashabiki wa timu hiyo ambao wameikosa kwa muda mrefu.

Mayanja ameyazungumza hayo tokea jijini Mbeya ambapo baadae, watakuwa na mechi dhidi ya maafande wa jeshi la magereza, Tanzania Prisons ili kusaka pointi tatu muhimu.

Hata hivyo, timu zote zitaingia uwanjani zikiwa na kumbukumbu ya kupoteza michezo yao ya mwisho ambapo, Simba walipoteza dhidi ya African Lyon, ikiwa ndio mechi yao ya kwanza kufungwa tangu msimu umeanza huku Prisons wakifungwa na mabingwa watetezi Yanga.

 “Sisi tunaangalia mbele hatuangalii nyuma, tunataka kuona tunapata ushindi kwenye mechi ya mwisho ya mzunguko wa kwanza ili tubaki kwenye nasafi ya kwanza kwenye ligi.”

“Mashabiki wasikate tama waendelee kuishangilia timu yao Simba ni timu yao wasikate tama kwa kupoteza mchezo huu.”

“Mwaka huu tunaomba Mungu tuweze kufikia malengo ya wanachama kwasababu wanachama wanamuda mrefu hawajaona kombe.”

Mechi nyingine itakuwa katika dimba la Mwadui Complex ambapo wenyeji, Mwadui FC watawakaribisha


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top