
KLABU ya Leicester City
imekata rufaa kupinga kadi nyekundu aliyopewa mshambuliaji wao tegemezi, Jamy
Vardy kwenye mchezo uliomalizika kwa sare ya goli 2-2 dhidi ya Stoke City siku
ya jumamosi.
Mshambuliaji huyo wa
timu ya taifa ya England alitolewa nje dakika ya 28 na mwamuzi Craig Pawson baada ya kumfanyia faulo mbili
mchezaji wa Stoke, Mame Diouf.
Taarifa kamili kutoka kwa mabingwa watetezi wa EPL zinasema timu imeamua
kukata rufaa hiyo kwani kwamuzi hakuwa sahihi na wanaamini ya kuwa rufaa yao
itasikilizwa siku chache za usoni.
Ikumbukwe ya kuwa Kwa Vardy, hii ni mara ya pili kupata kadi nyekundu
kwa msimu huu.
Post a Comment