
MCHEZAJI
wa Chelsea, Nemanja Matic amesema, Michy Batshuayi endapo atapewa nafasi kwenye
mchezo wa boxing day dhidi ya Bournemouth, huenda akampora namba mshambuaji wa
kutegemewa wa timu hiyo, Diego Costa.
Costa,
ambaye ni top-scorer kwenye EPL kwa sasa, ataokosa mchezo huo baada ya
kuonyeshwa kadi tano za njano na Batshuayi aliyejiunga na Chelsea akitokea Olympique
de Marseille amekuwa akihusishwa kuwa chaguo la Conte kwenye mchezo wa Boxing
day.
"Unapokuwa
na Costa kwenye timu yako na anacheza vizuri na kuscore magoli, ni vigumu sana
kupata namba mbele yake kama ni mzima na hana majeraha, lakini naamini Micky
anaweza kwani anajituma sana” Alisema Matic.
Batshuayi
ameshinda mara tatu kwenye michezo 13 aliyocheza Chelsea, na Matic anaamini
Micky ndiye mchezaji pekee wa kumrithi Costa.
"Bila
shaka amekuwa anamfaidi sana Costa na kujifunza vingi kutoka kwake, Ni sawa na
mimi miaka saba iliyopita, nilikuwa nafurahi na kujifunza vingi toka kwa Frank
Lampard, Michael Ballack na Michael Essien jinsi walivyokuwa wanacheza”
Aliongeza Matic.
"Hivyo, ni vizuri kwa micky
kutokana na kupata uzoefu toka kwa Costa na faida kubwa ikiwa ni kwamba huku bado
ana nafasi ya kucheza nae.”
Kwenye
mchezo huo, Kante pia atakuwa nje kwa kosa kama la Costa na hivyo Fabregas
akitarajia kuungana na Matic kwenye idara ya kiungo siku watakapowakaribisha
Bournamouth.
Post a Comment