SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: CHELSEA YAMRUHUSU OSCAR KUJIUNGA NA SHANGHAI NSIPG.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
KLABU ya Chelsea na Shanghai SIPG ya ya nchini China, zimekubaliana juu ya kumuuza Oscar kwenda kujiunga na ligi ya China maarufu k...
Oscar




KLABU ya Chelsea na Shanghai SIPG ya ya nchini China, zimekubaliana juu ya kumuuza Oscar kwenda kujiunga na ligi ya China maarufu kama Super League.

Oscar alithibisha hayo ya kuwa ni asilimia 90 makubaliano yamewshafanyika na akitarajiwa kuuzwa kwa paundi 60mil kwenye dirisha dogo la usajili mwezi ujao.

Oscar alijiunga na klabu ya Chelsea mwaka 2012 akitokea Internacional kwa kitita cha paund 25mil huku akipachika mabao 38 katika mechi 203.

Viongozi wa klabu ya Chelsea wamethibisha ya kuwa dili lake linakamilika mwezi January kwenye dirisha la usajili.

Oscar ambaye amekuwa akihaha kupata namba ya kuanza kwenye kikosi cha Conte, anatarajia kuungana na bosi wake wa zamani, Andre Villas-Boas huko Shanghai.

Hata upande wa Shanghai, nao pia wameshathibisha ya kuwa Oscar atajiunga nao muda si mrefu kwenda kuwaongezea nguvu.



Thamani ya uhamisho wa Oscar inatarajiwa kuingia kwenye rekodi za dunia ya kuwa atakuwa mmchezaji wa saba kununuliwa ghali zaidi duniani na atakuwa analipwa kiasi cha paundi 400,000 kila wiki.

Dirisha la usajili linatarajiwa kufunguliwa siku ya mwaka mpya na kufungwa tarehe 23 ya mwezi 
January.

Usajili wa Oscar unakuja siku chache baada ya uvumi wa nyota wa zamani wa timu ya Manchester City, Carlos Teves kujiunga na ligi ya China na kukadiriwa kuwa na mshahara mnono zaidi duniani.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top