SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SHAMTE FITI KUIKABILI TOTO, NGASSA KUENDELEA KUKAA BENCHI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
MENEJA wa kikosi cha Mbeya City, Godfrey Katepa amesema tayari Mbeya City wamejifua vyema kuwakabili Toto Africans ya jijini Mwanz...


dsc_0175

MENEJA wa kikosi cha Mbeya City, Godfrey Katepa amesema tayari Mbeya City wamejifua vyema kuwakabili Toto Africans ya jijini Mwanza kwenye mchezo namba 130 wa VPL utakaopigwa kwenye dimba la kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya hapo kesho.

Akizungumza na mtandao rasmi wa Mbeyacityfc.com Katepa amesema, “Hali ya kikosi chetu ni nzuri kabisa, hakuna mchezaji yoyote aliye majeruhi, Haruna shamte aliyekuwa na maumivu ya kifundo cha mguu amerejea kikosi baada ya matibabu ya siku kadhaa jopo la madaktari wetu wametuthibitishia kuwa yuko sawa tayari kwa mchezo wa kesho, ni wazi hakuna kinachotuzuia kushinda  mchezo huo” Katepa alisema.

Aidha, akizungumzia suala la Ngassa, Meneja amethibitisha ya kuwa hatokuwepo kwenye mchezo wa kesho kutokana na baadhi ya mambo kutokukamilika.

“Ni wazi ataukosa mchezo  huu, suala lake bado halijakamilika, jambo muhimu ni kuwa uongozi bado unaendelea kufanya mawasiliano na klabu ya Fanja  kuhakikisha  linakamilika ili aweze kuichezea timu yake mpya kwenye michezo ijayo, awali walitutumia TPO pekee, hivyo tunasubiri RELEASE LETTER kutoka kwao ili tuweze  kupata  ITC kwa mujibu wa taratibu, ilikuwa watutumia jana lakini mtu ambaye alipaswa kufanya hiyo kazi alikuwa nje ya Oman na anarejea  leo.

Hatuna msuguano wowote na Fanja kama inavyoripotiwa mawasialino kati yetu ni mazuri kama ilivyo kwa Tff na chama cha mpira cha Oman  hivyo  siku si nyingi suala hili litafikia mwisho alimaliza”

Mechi nyingine.
LEO;
African Lyon vs Yanga,
KESHO;
Mwadui vs Mbao FC.
Ndanda RC vs Mtibwa Sugar
Kagera Sugar vs Stand United.
Majimaji FC vs Azam FC



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top