SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: RANIERI AENDELEA KUIKOSOA ADHABU YA JAMY VARDY
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
CLAUDIO Ranieri amekosoa adhabu aliyopewa mshambuliaji wake Jamy Vardy ya kadi nyekundu na kukosa mechi tatu. Leicester walikata r...




CLAUDIO Ranieri amekosoa adhabu aliyopewa mshambuliaji wake Jamy Vardy ya kadi nyekundu na kukosa mechi tatu.

Leicester walikata rufaa ya adhabu hiyo ambayo hata hivyo rufaa yenyewe ilitupiliwa mbali na shirikisho la mpira wa miguu la England, FA.

Vardy, ambaye ni mfungaji bora wa Leicester msimu uliopita, alionyeshwa kadi nyekundu kwenye mechi dhidi ya Stoke na adhabu yake inaanza kuhesabiwa kwenye mechi ya jumatatu dhidi ya Everton.

"Kila mmoja hapa England na duniani kote alitazama mechi na kukubali ya kuwa ile wala haikuwa faulo ya kiasi hicho” Alisema Ranieri.

"Tulikata rufaa kwa sababu tulikuwa tunaamini ya kuwa tutapata haki yetu lakini tumekuwa disappointed kwa matokeo ya rufaa yetu na hii inamaanisha ya kuwa hata wachezaji wakifanya makosa basi sisi tusikate rufaa kwa sababu rufaa zetu huwa zinakatiwa” Aliongeza Ranieri.

Kuelekea mchezo boxing day, siku ya jumatatu, mabeki, Christian Fuchs na Robert Huth, nao pia watakuwa wakitumikia adhabu kwenye mechi ya Everton huku Midifilda, Danny Drinkwater yupo mashakani kama atacheza au laa kutokana na kusumbuliwa na kifundo cha mguu.

"Hata hivyo, hii itakuwa ni nafasi kwa wachezaji ambao huwa hawapati nafasi kwenye kikosi cha kwanza na kunishawishi ili niendelee kuwatumia kwenye michezo mingine.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top