
KLABU
ya KRC Genk, kupitia tovuti yao rasmi leo imetangaza kuachana na kocha wao Pete
Maes kutokana na kuwa na matokeo mabovu kwa siku za hivi karibuni.
Genk ambayo nahodha wa
timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Ally Samata anacheza, iko nafasi
ya 9 ikiwa imejikusanyia jumla ya pointi 25.
Maamuzi hayo yanakuja
siku moja kabla ya Genk kuwakaribisha mahasimu wao KAA Gent kwenye uwanja wao
wa nyumbani wa Crystal Arena.
Maes alijiunga na Genk
mwaka 2015 akitokea klabu ya Lokeren ya nchini Ubelgiji.
Post a Comment