
TIMU
ya KRC Genk leo ilikuwa katika dimba la Luminus Arena kuwakaribisha mahasimu
wao KAA Gent bila ya aliyekuwa kocha wao Peter Maes na kuibuka na ushindi wa
goli 2-0.
Magoli ya Genk yamewekwa
kimiani Aljandro Pozuelo dakika ya 19 ya mchezo na Nikolas Karelis, aliyefunga
kwa mkwaju wa penalty dakika ya 25.
Genk waliokuwa wakicheza
chini ya mkufunzi msaidizi wa zamani wa klabu ya Manchester United, Albert
Stuivenberg bado wameendelea kusalia kwenye nafasi ya 9 huku wakiwa na pointi
28 wakati vinara wa ligi hiyo, Club Brugge wakiwa na pointi 43 lakini wakiwa
wamecheza mechi moja Zaidi ya Genk.
Nahodha wa timu ya taifa
ya Tanzania, Mbwana Samatta aliingia dakika ya 51 akichukua nafasi ys Kaleris.
Post a Comment