
HUU
ndio
msimu bora sana kwa klabu ya Chelsea walio chini Antonio Conte, baada ya
kuendeleza rekodi yao ya kutokupoteza mchezo kwenye ligi kuu ya EPL.
Ushindi wa jana wa
Chelsea wa 3-0 dhidi ya FC Bournamouth ulikuwa ni ushindi wa 12 mfululizo kwa
timu hiyo kushinda.
Lakini kikubwa Zaidi ni ule mwendelezo wa
wachezaji kuendelea kujiwekea rekodi zao ndani ya klabu ya Chelsea.
Eden Hazard jana
alifanikiwa kufunga bao moja na kufikisha idadi ya magoli 50 na akiingia kwenye
rekodi ya watu 6 waliowahi kufunga mabao Zaidi ya 50.
Baadhi ya wachezaji wa
Chelsea waliowahi kufunga magoli Zaidi ya 50 ni Lampard, Drogba, Hasselbaink, Zola na Gudjohnsen.
Hatimaye Hazard ameingia kwenye kundi hili na anaonekana kuwa na uwezo
wa kufika mbali zaidi kwasababu bado ana nafasi ya kucheza na kufunga magoli
mengi zaidi.
Post a Comment