
RAIS
wa
Zambia, Edgar Lungu ameliagiza shirikisho la mpira wa miguu la nchi hiyo
kuajiri makocha wazawa wa timu ya taifa ya Zambia, Chipolopolo.
Shirikisho hilo linalofahamika kama FAZ,
limekuwa likitafuta wataalamu kwa ajili ya kuwapa tenda hiyo lakini pia hata
kuwa na interview na baadhi ya makocha wa kigeni.
Aliyekuwa kocha wa
zamani wa timu ya taifa ya Africa Kusini, Gordon Igesund amekuwa akihusishwa na
kibarua hicho baada ya kuwavutia watendaji wa shirikisho hilo kwenye mahojiano.
Lakini Lungu aliwaambia
maafisa wa shirikisho hilo kwamba wasahau kuwaajiri makocha wa kigeni na badala
yake wawaajiri makocha wazawa,
“Sahauni juu ya makocha
wakigeni, Tunaweza kupata mafanikio na makocha wa ndani ya nchi” Alisema Lungu.
Lungu pia alitoa msaada
wake kwa kocha wa muda wa Chipolopolo, Wedson Nyirenda, ambaye aliteuliwa kama
mbadala wa George Lwandamina mwezi uliopita, akisema amefanya vizuri kwa muda
mchache alioachiwa timu.
Hayo yamekuja baada ya
Zambia kupoteza mchezo wake dhidi ya timu ya Nigeria kwa 2-1 mchezo wa kuwania
kufuzu fainali za kombe la dunia za mwaka 2018, nchini Urusi.
Hata hivyo, licha ya
Chipolopolo kufungwa mchezo wa kwanza, Lakini Lungu anaamini bado Zambia ina
nafasi ya kufuzu fainali hizo.
Post a Comment