
SIKU
chache zilizopita tayari kulishaanza kuibuka kwa maneno ya vijembe kwa kocha wa
Ufaransa, Tayari yalishaanza maneno kwa kocha wa Ufaransa Didier Deschamps kuwa
uwezo wa Paul Pogba umeporormoka sana tangu ajiunge na Mnchester United kwa dau
nono la Pauni miln 89.

Huenda
hayo yakapotea baada ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 kuipatia timu yake
ya taifa goli la ushindi, walipokutana na timu ya taifa ya Uholanzi kwenye
mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2018
Paul
Pogba alifunga bao hilo kwa umbali wa mita 30 ambalo lilimshinda golikipa wa
Everton Maarten Stekelenburg licha ya kujaribu kuupangua mpira huo.
Golikipa
huyo mdachi alipambana kadri alivyoweza ili kuzuia shuti la Pogba lakini
hakuweza kufanya kile ambacho alitarajia kukifanya na hatimaye kuzishuhudia
nyavu zake zikicheza.
Sasa
huenda mashabiki wa Manchester United wakawa na matumaini mapya ya kumuona
Pagba akifunga magoli mengine kama hayo akiwa kwenye klabu yake ya Old Trafford
Post a Comment