
MLINZI wa kutumainiwa wa timu ya Real Madrid
na timu ya taifa ya Hispania, aliumia kwenye mchezo wa kufuzu fainali za kombe
la dunia dhidi ya Albania, ambapo
Hispania ilishinda 2-0.
Ramos 30,
alitolewa nje dakika ya 80 baada ya kushindwa kuendelea na mchezo huo.
Klabu yake
ya sasa Real Madrid imethibisha ya kuwa, Nahodha huyo wa Hispania amesikitishwa
sana na jeraha hilo la goti litakalomweka nje kwa zaidi ya majuma manne.
Aidha, imeripotiwa
kuwa, Ramosi atakuwa nje kwa takribani mwezi mmoja ambapo ataikosa baadhi ya
mechi za ligi ukiwemo ule wa mahasimu wao Atletico Madrid.
Lakini pia
Ramos ataukosa mtanange wa ligi ya mabingwa dhidi ya Legia Warsaw na akiwa
mashakani kucheza mechi dhidi ya Macedonia ya kufuzu fainali za kombe la dunia
tarehe 12 ya November.
Post a Comment