
MCHEZO wa ligi kuu Tanzania bara kati ya Azam na Yanga umemalizika kwa timu hizo kutoshana nguvu ya bila kufungana katika dimba la Uhuru jijini Dar es salaam.
Huu unakuwa mchezo wa tatu kwa Yanga kutoka sare huku ikiwa imepoteza mchezo mmoja na kushinda michezo minne na kujikusanyia pointi 15.
Kwa upande wa Azam huu unakuwa mchezo wa tatu kutoka sare huku wakiwa wamefungwa michezo mitatu na kushinda michezo mitatu.
Matokeo
Ruvu 1-0 Mbeya City
Mtibwa Sugar 0-0 Tanzania Prisons
Toto Africans 1-2 Majimaji FC
Post a Comment