SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SIMBA YAILAZA POLISI DODOMA MCHEZO WA KIRAFIKI.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
KLABU ya Simba imeibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya timu ya Polisi Dodoma , mchezo wa kirafiki uliopigwa katika dimba la jamhuri, mj...
Said Ndemla (kulia) akishangilia goli lake na Haji Ugando (kushoto) wakati wa mechi dhidi ya Polisi Dodoma kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma


KLABU ya Simba imeibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya timu ya Polisi Dodoma , mchezo wa kirafiki uliopigwa katika dimba la jamhuri, mjini Dodoma.

Magoli ya Simba yamewekwa kimiyani na Abdi Banda 45+2 akiunganisha kwa kichwa mpira wa adhabu uliopigwa na kiungo, Mwinyi Kazimoto huku goli la pili likifungwa na Said Ndemla akliyepiga shuti kali la umbali w mita 22 na kumshinda mlinda mlango wa Polisi Dodoma dakika ya 60 na mpaka mwamuzi anapuliza filimbi ya mwisho, ubao ulikuwa unasomeka Simba 2-0 Polisi Dodoma.

Mchezo huo ulikuwa ni maalumu kwa ajili ya kuunga mkono adhma ya serikali ya kutaka kuhamishia makao makuu ya serikali hiyo mjini Dodoma.

IMG_0113

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Tulia Akson alikua mgeni wa heshima kwenye mechi hiyo ambapo aliambatana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo Mh. Nape Nnauye pamoja na viongozi wengine wa serikali ya mkoa wa Dodoma

Mwinyi Kazimoto (kushoto) alionesha kiwango cha juu kwenye mchezo huo kwa kutengeneza nafasi za kufunga ambazo hazikutumiwa vyema na Blagnanon na Lyanga


Simba ilitumia wachezaji wake wengi ambao hawapati nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo kutokana na wachezaji wengi wa timu hiyo kuitwa kuzitumikia timu zao za taifa. Ibrahim Ajib, Jonas Mkude, Mohamed Hussein, Shiza Kichuya, Muzamiru Yassin wote wapo Nigeria kwenye kikosi cha Stars wakati Laudit Mavugo yeye akiwa kwenye timu yake ya taifa ya Burundi

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top