
DROO ya raundi ya nne ya Kombe la Ligi
nchini England maarufu kama EFL Cup imefanyika Usiku wa kuamkia leo ambapo timu
mbalimbali zimewajua wapinzani wao.
Katika
droo hiyo imeshuhudiwa mahasimu wawili wa jiji la Manchester yaani Manchester
na United wakikutana kwenye mchezo utakaofanyika Oktoba 24.
Hii
inakuwa mara ya pili kwa United na City kukutana mara baada ya hapo awali
kukutana kwenye mchezo wa Premier League ambapo, Man City walishinda mabao 2-1
kwenye mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Old Trafford.
Katika
mchezo huo Manchester United kwa mara nyingine tena watakuwa wenyeji dhidi ya
mahasimu wao Manchester City.
Hamu
kubwa ya mashabiki wa klabu ya Manchester United ni kuona ni kwa kiasi gani
timu yao wangependa ikisawazisha makosa yaliyojitokeza kwenye mchezo wa ligi kuu
ambao Manchester United walikubali kipigo cha mabao 2-1
Post a Comment