Baada ya klabu ya Everton kumruhusu
beki wao tegemezi John Stones kujiunga na klabu ya Mancity, timu hiyo yenye
makazi yake huko Merseyside imekamilisha dili la usajili wa beki wa klabu ya
Swansea City Ashley Williams kwa kitita kinachosemekana kuwa ni pauni 12mil
Williams, 31, anakuwa
mchezaji wa tatu kununuliwa na kocha mpya wa klabu hiyo Ronaid Koeman, baada ya
kuwachukua Idrissa
Gueye mchezaji kiungo wa Senegal na
golikipa Maarten Stekelenburg.
Lakini pia klabu hiyo
ya Everton bado wapo kwenye mazungumzo na kiungo wa klabu ya Crystal Palace, Yannick
Bolasie na beki wa klabu ya Sunderland, Lamine Kone.
"Ninaamini klabu
inakwenda kwenye uelekeo sahihi," Alisema Williams.
Beki huyo ambae
amesaini kandarasi ya miaka mitatu kuitumikia klabu hiyo amesema alikuwa anawaza siku moja kufanya
kazi na kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi Koeman.
"Amekuwa ni moja
ya watu wenye uwezo wa kuwaunganisha wachezaji kwa pamoja, hivyo nikitazamacho
sasa mbeleni ni kujifunza vingi chini yake” Williams
aliuambia mtandao rasmi wa klabu hiyo.
Awali klabu ya Swansea
ilikataa ofa ya pauni 10mil kutoka Evertona na sasa wamepokea pauni 12mil baada
ya kumuuza mchezaji wao tegemezi kwa matajiri wa jiji la Manchester, klabu ya
Manchester City kwa pauni 47mil.
Williams alikuwa moja
ya wachezaji wa kikosi cha timu ya taifa ya Wales kilichotolewa katika hatua ya
nusu fainali ya mataifa ya ulaya na timu ya taifa ya Ureno, lakini pia Williams
hakucheza mechi yeyote ya kirafiki kutokana kuwa na likizi ndefu baada ya
mashindano ya EURO ya Ufaransa.
Williams ameichezea
Swansea City kwa takribani miaka 8 tangu ajiunge nao mwezi march kwa pauni 300,000 akitokea klabu Stockport na
kucheza mechi 300.
Mbali na raia wa Ivory Coast
Kone 23, anayefukuziwa na klabu hiyo, lakini pia wamesema wangependa kuendelea
kuw na mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ubelgiji Lukaku licha ya klabu yake ya
zamani ya Chelsea ikionekana kutaka kumrudisha.
Post a Comment