
WAPINZANI wa timu Yanga, klabu ya
FC MO Bejaia ya nchini Algeria leo imefanya mazoezi katika uwanja mkuu wa taifa
jijini Dar es salaam mchezo wa hatua ya makundi ya kombe la shirikisho barani
Africa.
Mchezo huo utafanyika
siku ya kesho, majira ya kuanzia saa kumi za jioni kwa majira ya Africa
mashariki ukiwa ni mchezo wa tano kwa timu zote mbili.
Wenyeji, klabu ya Yanga
wanaingia kwenye mchezo huo, wakiwa wanaburuza mkia katika msimamo wa kundi A
wakiwa na point poja pekee baada ya kucheza michezo minne na kukubali kufungwa
michezo itatu, huku wakitoka sare ya mchezo mmoja dhidi ya klabu ya Medeama ya
nchini Ghana.

Klabu ya MO Bejaia wao
wanaingia kwenye mchezo huo, wakiwa wa tatu kwenye msimamo wa kundi hilo baada
ya kukubali kufungwa mechi moja huku wakitoka sare mechi mbili na kushinda
mechi moja.
Kwa upande wa Yanga,
kupitia kwa kocha msaidizi wa klaabu hiyo, Juma Mwambusi, alipokuwa anaongea na
msemaji wa TFF Alfrd Lucas, amesema, Yanga imejiandaa vizuri kuelekea mchezo
huo, japo kuna baadhi ya wachezaji wao muhimu.
“Sisi tupo vizuri,
tumejiandaa vizuri kabisa japo tutawakosa wachezaji wetu muhimu kama vile
Donald Ngoma yeye ana kadi mbili za njano na Mwashiuya ambae ana maradhi ya
muda mrefu” Mwambusi Alisema.
Kwa jedwali la kundi A
linasomeka hivi.
Timu… MP
W D L G PNTS
1. MAZEMBE 4 3 1
0 5:1 10
2. MEDEAMA 4 1
2 1 5:5
5
3. MO BEJAIA 4 1
2 1
1:1 5
4. YOUNG AFRICAN 4 0
1 3 2:6
1
Post a Comment