
TIMU ya Manchester United itamkosa
mchezaji wake iliyemsajili kwa Pauni Milioni 100, Paul Pogba katika mchezo wa
kwanza wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Bournemouth Jumapili.
Pogba amefanya mazoezi na kikosi cha kocha Mreno, Jose Mourinho leo, lakini hatasafiri kwenda Uwanja wa Vitality kwa sababu atakuwa anatumikia adhabu ya kadi.
Chama cha Soka England (FA) kimethibitisha kwamba Mfaransa huyo alionyeshwa kadi za njano katika mechi za mwisho za Kombe la Italia, msimu uliopita.
Kurejea kwa Pogba katika klabu yake ya
zamani, Manchester United, kulithibitishwa rasmi mapema Jumanne, lakini habari
za kutocheza dhidi ya Bournemouth zinakuja kama za kushitukiza.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23
alionyeshwa kadi ya njano katika ushindi wa Juventus wa 1-0 dhidi ya AC Milan
kwenye fainali ya Coppa Italia mwezi Mei, hiyo ikiwa kadi yake ya
pili mfululizo kwenye mashindano hayo.
BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE inafahamu
kwamba kwa mujibu wa sheria, Pogba anapaswa kukosa mchezo mmoja baada ya kadi
hizo na sasa adhabu hiyo inahamia Ligi Kuu ya England.
FA
imesema Xherdan Shaqiri pia alikutana na mazingira hayo wakati kiungo huyo wa
Uswisi alipohamia Stoke City mwaka 2015 kutoka Inter Milan
MECHI TANO ZA MWANZO ZA MAN UTD LIGI KUU ENGLAND
Agosti 14: Bournemouth (ugenini)
Agosti 19: Southampton (nyumbani)
Agosti 27: Hull (away)
Septemba 10: Man City (nyumbani)
Septemba 18: Watford (ugenini)
Post a Comment