
MCHEZO wa raundi ya tano wa kombe la shirikisho barani Africa uliopigwa jijini Dar es salaam, umemalizika kwa klabu ya Yanga kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya klabu ya MO Bejaia ya nchini Algeria.
Tambwe ndie aliyepachika bao hilo la ushindi akimalizia mpira
wa faulo uliopigwa na Thaban Kamusoko dakika ya pili ya kipindi cha kwanza.
Ushindi huo bado hauwezi kuisogeza popote klabu ya Yanga, kwani bado itaendelea
kuburuza mkia huku akiwa na pointi nne pekee, nyuma ya Mo Bejaia na Medeama
walio na pointi tano wote kwa pamoja huku Mazembe akiwa kinara wa kundi hilo
akiwa na pointi 10 kibindoni.
Japo nafasi ya klabu ya yanga ni finyu mno, bado wana nafasi
ya kusonga mbele endapo watashinda mchezo wao wa mwisho dhidi ya timu ya TP
Mazembe ya nchini Congo.
Hizi ni hesabu tu ambazo wakati mwingine huwa hazina nafasi
sana katika mchezo wa soka kwani wakati unataka kupata matokeo Fulani, huku
unakuwa unmwombea mpinzani wako mabaya, kiukweli ni hesabu ambazo huwa hazina
kichwa wala miguu.
Kikubwa ambacho kipo kwa sasa ni kukubali ya kuwa Yanga
walichelewa sana, kama wangepata matokeo katika michezo ya awali, hakika leo
angekuwa anachekelea, sasa badala yake, huu mchezo unabaki kama kukamilisha
ratiba lakini pia wao kuonyesha ya kuwa walikuwa wamekata tamaa,waliuita ni
mchezo wa kirafiki.
Post a Comment