
Mabingwa wa ligi ya Ufaransa, klabu ya Paris st-Germain,
wamefanikiwa kuinasa sahihi ya mchezaji wa Real Madrid Jesse Rodrguez kwa
thamani ambayo haiuwekwa wazi.
Jesse ametia kandarasi ya miaka mitano kuitumikia klabu hiyo
ya nchini Ufaransa.
Jesse 23, raia wa Hispania alijiunga na mabingwa hao wa
zamani wa Laliga tangu akiwa na miaka 14 na alikuwa kwenye kikosi kilichochukua
ubingwa wa Uefa mwaka 2014 na 2016.
Jesse anaungana na aliyekuwa kocha wa klabu ya Sevilla Unai
Emery aliyechukua nafasi ya Laurent Blanc ambae msimu wake ulikuwa umemalizika.
‘‘Litakuwa ani jambo jema sana kucheza chini ya mwalimu Unai
Emery ambae aliiongoza klabu ya Sevila kwa mafanikio makubwa na naamini na mimi
nitakuwa na mafanikio hapa PSG” Alisema Jesse.
Post a Comment