SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: TAMTHILIA YA POGBA YAELEKEA UKINGONI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Juventus na timu ya taifa ya Ufaransa, Paul Pogba amewasili katika viunga vya Calinton kwa ajili ya kuf...
Paul Pogba arrives at Manchester United's training ground

Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Juventus na timu ya taifa ya Ufaransa, Paul Pogba amewasili katika viunga vya Calinton kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya afya na kabla hawajafanya makubaliano ya maslahi ya mkataba wake na klabu.

Pogba aliuzwa mwaka 2012 kwa pauni 1.5mil kwa mabingwa wa ligi ya Italia, klabu ya Juve, lakini anatarajia kurudi Trafford kwa kitita cha pauni 89m ikiwa ni sawa na Euro 105mil

Pogba anatarajiwa kuvunja rekodi ya ada yake ya uhamisho, ambapo kabla yake, rekodi hiyo ilikuwa inashikiliwa na mchezaji wa Real Madrid Gareth Bale aliyesajiliwa toka klabu ya Totenham ya Wingereza kwa pauni 85mil.

Pogba aliondoka Old Trafford baada ya kushindwana na aliyekuwa kocha wake Sir Alex Fugerson kutokumhakikishia namba, na wakala wa Pogba Mino Raiola akamtafutia klabu mpaka leo anarudi ManU kama malaika kwa gharama ya juu Zaidi.

Siku za nyuma, kocha wa klabu hiyo alipoulizwa juu ya ujio wa Pogba, alisema bado alikuwa hayuko tayari kuzungumzia wachezaji wa timu nyingine, lakini baada ya mchezo wa jana wa ngao ya hisani MaU kuifunga Leicester goli 2-1, Morinho akaibuka na kusema nilikuwa nasubiri mchezo huu uishe, na bila shaka kesho [leo] Pogba atakuja kufanya vipimo vya afya.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top