SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: SAMATTA ATUPIA MBILI GENK IKISHINDA 3-0
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
NAHODHA wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, na mshambuliaji wa klabu ya KRC Genk, Mbwana Ally Samatta ameendelea kufanya vye...





NAHODHA wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, na mshambuliaji wa klabu ya KRC Genk, Mbwana Ally Samatta ameendelea kufanya vyema baada ya hapo jana kuiongoza timu yake ya Genk kushinda ushindi mujarabu wa goli 3-0 dhidi ya Lokeren.

Samatta alianza kufunga goli la kwanza dakika ya 34 kipindi cha kwanza kabla ya kufunga bao jingine dakika nne baadaye.

Bao la tatu la Genk limefungwa na Leon Bailey dakika ya 48 kipindi cha pili na magoli hayo yakidumu kwa dakika zote.

Samatta alipumzishwa dakika ya 73 kumpisha mshambuliaji mwenye asili ya Ugiriki Nikos Karelis.

Kwa ushindi huyo, klabu ya Genk inapaa hadi nafasi ya nne kwa kuwa na pointi  7 kuku mbele yake zikiwepo timu kama, Zulte Waregen, Anderlecht na Spoting Chalrelou.
.

 

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top