SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: WAZIRI WA MICHEZO AKABIDHIWA UWANJA WA UHURU.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
  Picha na Salehe Jembe. BAADA ya ukarabati wa miaka mitatu wa uwanja wa uhuru, maarufu kama shamba la bibi, na wakandarasi ...


 
Picha na Salehe Jembe.

BAADA ya ukarabati wa miaka mitatu wa uwanja wa uhuru, maarufu kama shamba la bibi, na wakandarasi wachina, leo uwanja huo umekabidhiwa mikononi mwa serikali.

Kampuni ya Beijing Construction Engineering Group (BCEG) ya nchini China ambayo ilikuwa ikisimamia marekebisho ya uwanja huo chini ya meneja wake mkuu, Cheng Longhai, walimkabidhi Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye katika hafla fupi iliyofanyika uwanjani hapo, mapema hii leo. 

 

 

 Akizungumza baada ya kukabidhiwa uwanja huo Nape alisema: “Ni jambo la busara kwa kila atakayeutumia uwanja huu kuwa mlinzi kwa mwenzake ili kulinda miundombinu yake ili udumu kwa miaka mingi zaidi kwani hii ni hazina yetu sote.”

Wakati huohuo, mbunifu wa michoro ya uwanja huo, Aloyse Peter Mushi, alisema: “Uwanja huu unaingiza watu waliokaa elfu 23, lakini wakikaa kwa kubanana wanafika elfu 25, tulianza marekebisho haya mwaka 2013, na tunashukuru leo hii umekamilika na serikali kukabidhiwa”

Hivyo, baada ya marekebisho hayo, uwanja huo utatumika kwenye mechi mbalimbali, zikiwemo zile za ligi kuu VPL.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top