
Timu ya taifa ya Equetorial Guinea ya
wanawake, imefungiwa kushiriki katika fainali za kombe la mataifa ya Africa kwa
upande wa wanawake katika fainali tatu mfululizo kwa kumtumia mchezaji ambae
hakustahili kucheza.
Mwezi Agosti, shirikisho la mpira la
dunia FIFA, lilibaini kuwa mchezaji Camila
Maria do Carmo Nobre de Oliveira alikuwa anamiliki paspoti mbili za kusafiria
na vyeti viwili vya kuzaliwa vyenye tarehe tofauti, na kufuatia hayo, wakawa
wametolewa katika hatua za mwanzoni za kufuzu michezo ya Olympic za mwaka 2020.
Shirikisho la mpira barani Africa, CAF limewaadhibu tena
taifa hilo la Equetorial Guinea kwa kosa hilo hilo.
Kupitia mtandao rasmi wa shirikisho hilo, viongozi wa CUF
wamesema hayo yamefanyika baada ya taifa la Mali kupinga matokeo ya Equetorial
Guinea kushinda goli 3-2 yao katika raundi ya mwisho ya kufuzu fainali za kombe
la mataifa.
Camila Nobre do Carmo Oliviera alipangwa kwenye mechi dhidi
ya mali, michezo iliyofanyika tarehe 6 na 10 ya mwezi April. Kufuatia uchunguzi
wa CUF ulibaini ya kuwa mchezaji huyo alikuwa amesajiliwa kwa jina la Camila
Maria Nobre Carmo katika fainali za AFCON kwa wanawake za mwaka 2014
zilizofanyika huko Namibia huku tarehe yake ya kuzaliwa ikiwa ni 7/10/1994 na
kwa mashindano yam waka huu, cheti chake cha kuzaliwa kikiwa kinasomeka kama
alizaliwa tarehe 10/6/1988 huku kikiwa na jina la Camila Nobre do Carmo
Oliviera".
Shirikisho la mpira chini humo limekiri kuwa tatizo hilo
limeweza kujirudia, Camila Nobre do Carmo Oliviera ameweza kufungiwa miaka
mitatu lakini pia na taifa kwa upande wa timu ya wanawake wakati nafasi ya E
Guinea itachukuliwa sasa na timu ya taifa ya Mali katika michuano hiyo itakayofanyika
nchini Cameroon kuanzia November 19
mpaka December 3.
Post a Comment