
Mchezaji wa kimataifa wa klabu ya Manchester City na timu ya
taifa ya Ubelgiji Kevin De Bruyne amesisitiza kwamba kocha wa klabu hiyo raia
wa Hispania Pep Guardiola atachukua muda mrefu kuleta falsafa na mbinu zake
katika klabu hiyo ya jijini Manchester.
De Bruyne, 25 ni moja ya wachezaji wa klabu ya Manchester City
walioitwa katika timu za taifa kwenye mashindano ya EURO ya mwaka huu na
mashindano ya Copa America, ni yeye pekee aliyerejea katika mapumziko yao ya
muda mrefu na kujiunga na timu hiyo katika mazoezi ya Alhamisi
‘‘Amebadilisha baadhi ya
vitu vichache klbu hapa” Alisema De Bruyne alipokuwa akihojiwa na kituo cha TV
cha skysports.
‘‘Bila shaka ndio itamchukua muda kidogo haswa kwa wale ambao
wamechelewa kujiunga na kikosi hicho. Ni vigumu sana kujenga timu wakati watu
wengine wakija nje ya muda baada ya EURO pamoja na Copa America”
Kocha Guardiola raia wa Hispania aliacha kazi ya kuifundish
klabu ya Bayern Munich na kuingia mkataba wa kukinoa klabu hicho cha Manchester
City akichukua nafasi ya Manuel Pelegrin aliyetimuliwa.
Matajiri hao wa jijini Manchester wataanza kampeni yao ya
kulisaka kombe la EPL kwa mchezo dhidi ya klabu ya Sunderland katika uwanja wao
wa Etihad siku ya tarehe 13 mwezi huu.
Post a Comment