
Siku
chache baada ya matajiri wa jiji la Manchester, klabu ya manchester city kukamilisha
dili la usajili wa mjerumani Leroy Sane toka klabu ya Shakle 04 ya Ujerumani,
klabu hiyo tena imefanikiwa kumpa kandarasi ya miaka 5 mchezaji kinda toka
nchini brazil, Gabriel Jesus kwa kitita cha pauni milion 27 akitokea klabu ya
Palmeiras.
Man city
wamempa Jesus mkataba huo wa miaka mitano lakini ataendelea kubaki katika klabu
ya Palmeiras mpaka mwisho wa msimu wa ligi ya Brazil na atajumuika na kikosi
cha matajiri hayo mnamo mwezi december mwaka huu.
Jesus
alichaguliwa kama mchezaji bora chipukiziwakati akiwa Palmeiras na kiifungia
klabu hiyo magoli 26 katika mechi 67 alizocheza na hadi sasa akiwa kama
mfungaji bora katika ligi hiyo.
Man city
wameipiku Barcelona waliokuwa wanataka kumsajili kinda huyo anayetarajiwa
kuoingoza timu yake ya taifa ya Brazil katika mashindano ya Olimpic
yanayofanyika mchini humo.
Mpaka
sasa matajiri hao wametumia karibu ya pauni milion 100 kwa kuwasajili wachezaji
kama vile Norito, Gundogan Sane pamoja na kinda huyo wa brazili Gabriel Jesus.
Post a Comment