SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: REAL MADRID MABINGWA, SUPER-CUP.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mchezo wa Super Cup umemalizika kwa klabu ya Real Madrid kutwaa kombe hilo kwa ushindi wa goli 3-2 dhidi ya klabu ya Sevilla, timu zo...






Mchezo wa Super Cup umemalizika kwa klabu ya Real Madrid kutwaa kombe hilo kwa ushindi wa goli 3-2 dhidi ya klabu ya Sevilla, timu zote za nchini Hispania.

Mchezo wa Super-Cup huwakutanisha mshindi wa klabu bingwa barani ulaya ambao kwa msimu wa mwaka 2015-2016 walikuwa klabu ya Real Madrid dhidi ya mshindi wa EUROPA ambao walikuwa ni Sevilla.

Marco Asensio ndiye aliyekuwa wa kwanza kuwanyanyua mashabiki wa klabu ya Real Madrid baada ya kuipatia timu yake bao la uongozi dakika ya 21, goli ambalo lilidumu mpaka dakika ya 41, Franco Vazquez kuisawazishia Sevila na Yevheniy Konomlyanka kupachika goli la pili dakika ya 71 kabla ya Segio Ramos kuukwamisha mpira wavuni na kufanya dakika 90 za mwamuzi kupulizwa, wakiwa wamefungana 2-2

Ilimlazimu mwamuzi wa mchezo huo kuongeza dakika 30 ambapo ndizo zilikuwa dakika chungu kwa timu ya Sevila baada ya kukubali kufungwa goli dakika ya 119 na mlinzi wa kulia wa Real Madrid, Carvajal kuukwamisha mpira wavuni kuipatia Real Madrid goli la ushindi.

Karim Benzema alipaswa kusubiri mpaka Morata alipotolewa na ndipo alipoingia huku Gareth Bale kuukosa mchezo huo pamoja na Cristiano Ronaldo nae kuukosa mchezo huo akiwa bado anaendelea kuuguza jeraha lake alilolipata dhidi ya timu ya taifa ya Ufaransa katika mchezo wa fainali ya mashindano ya Euro yaliyofanyika nchini Ufaransa.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top