
Claudio Ranieri
ameongeza mkataba wa kuendelea kuitumikia klabu ya Leicester City, mabingwa wa
EPL kwa mkataba wa miaka minne.
Raineri, 64, raia wa
Italia, aliiongoza Leicester, The Fox kutwaa kombe la EPL ikiwa ni mara ya
kwanza kwa klabu hiyo kuandika historia hiyo huku nayeye Ranieli akitengeneza
historia yake.
Ranieri anaungana na
wachezaji muhimu wa klabu hiyo Kasper Schmeichel, Wes Morgan na Jamie Vardy
ambao pia wameongeza mkataba kuendelea kuitumikia klabu hiyo ya England.
“Nguvu ambayo ipo hapa,
kutoka kwa wamiliki na uongozi kwa ujumla, kwa wachezaji na mashabiki ni jambo
zuri sana” Ranieri alisema.
“Msimu ulioisha, ule
moyo, pamoja na kujituma kwetu, kulitupelekea kupata mafanikio haya tuliyonayo.
Kama tutaendelea kujituma kwa bidii, kuendeleza ile ari yetu na kuendelea
kupigana kwa mioyo yetu sote kwa pamoja,
ninaamini tutaendelea kuwa wa mafanikio wote kwa pamoja” Alisema.
Leicester
waliopigwa na Manchester United kwenye mchezo wa Ngao Ya Hisani 2-1 siku ya
jumapili, watakuwa na kibarua kizito kucheza mchezo wake wa kwanza kwenye ligi
siku ya jumapili, ambapo watasafiri kuwafuata klabu ya Hull City iliyopanda
daraja msimu huu.
Makamu
mwenyekiti wa klabu hiyo Aiyawatt Srivaddhanaprabha alisema, “Miezi 12
iliyuopita, tulimleta hapa klabuni mtu ambaye tulihisi angetufikisha kwenye
hatua nyingine ambayo tulikuwa tunaiwaza muda mrefu. Uwezo wake na kile
alichotuzawadia ni zaidi ya hiki tulichokipata”
Nahodha
wa Leicester, Wes Morgan, ambae pia ameongeza mkataba wake mpaka mwaka 2019
amesema, “Kocha ranieri kuongeza mkataba ni habari njema sana, na kuongeza
kwamba alikuwa ana msimu bora sana na mafanikio walioyapata msimu uliomalizika,
ni furaha ya wote, na vijana wapo tayari kumpa tena sapoti kubwa kuyafikia
malengo yake”
Post a Comment