SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: RATIBA YA KLABU BINGWA NA SHIRIKISHO BARANI AFRICA.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
SHIRIKISHO la mpira barani Africa, CUF, limeweka hadharani ratiba ya michezo ya nusu fainali ya kombe la klabu bibgwa barani Africa...


Mamelodi Sundowns

SHIRIKISHO la mpira barani Africa, CUF, limeweka hadharani ratiba ya michezo ya nusu fainali ya kombe la klabu bibgwa barani Africa pamoja na zile za shirikisho.

Kwa upande wa Ligi ya Mabingwa, ambapo bingwa wa michuano hiyo anatarajiwa kujizolea kitita cha dola za Kimarekani Milioni 1.5 pamoja na kupata tiketi ya kucheza Klabu Bingwa ya Dunia, Mabingwa wa zamani Zamalek ya Misri ambao wamechukua kombe hilo mara tano watamenyana na vigogo wa Morocco, Wydad Casablanca kuwania kutinga fainali.

Ikumbukwe kuwa Zamalek watakuwa na ari kubwa kutokana na kuikosa hatua hii kwa takriban miaka 10, baada ya mara ya mwisho kufanya hivyo mwaka 2005. 

Kwa upande wa klabu ya Zesco United ya Zambia, ambao ni mara yake ya pili kufika hatua hii, itakuwa na kibarua kizito kumenyana na klabu ya Africa Kusini, Mamelod Sundowns, timu ambao kwenye michuano ya mwaka huu imeonyesha upinzani mkali sana.

Kwa upande wa mechi za shirikisho, TP Mazembe itamenyana na Etoile du Sahel ya Tunisia, huku MO Bejaia ya Algeria wataumana uso kwa uso na waarabu wenzao wa FUS Rabat ya Morocco.

Klabu Bingwa
Sept 16-18, 2016
Zamalek (Misri) Vs Wydad Athletic Club (Morocco)
Zesco (Zambia) Vs Mamelodi Sundowns (Afrika Kusini)
Kombe la Shirikisho
Sept 23-25, 2016
TP Mazembe (DRC) Vs Etoile du Sahel (Tunisia)
MO Bejaia (Algeria) Vs FUS Rabat (Morocco)

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top