SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: Mkuu wa FIFA wa zamani Sepp Blatter mahakamani tena
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
  RAIS wa zamani wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA Sepp Blatter, anawasilisha rufaa yake ya mwisho mahakamahi hii leo...


 


RAIS wa zamani wa shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA Sepp Blatter, anawasilisha rufaa yake ya mwisho mahakamahi hii leo dhidi ya marufuku aliyowekewa ya michezo na michezo kwa kukiuka madili. 

Bw Blatter anahudhuria mahakamani kusikiliza kesi hiyo inayoendeshwa na mahakama ya usuluhishi wa mizozo michezoni nchini Uswizi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Lausanne, amejielezea kama mtu mwenye matumaini. 

Bw Blatter aliwekewa marufuku hiyo mwezi Disemba mwaka jana kwasababu aliidhinisha malipo ya zaidi ya dola milioni mbili kwa mkuu wa zamani wa soka barani Ulaya , Michel Platini, miaka mitano iliyopita. 

Mwezi Mei, Bw Platini alishindwa kushawishi kuondolewa kwa marufuku dhidi yake, ingawa ilipunguzwa kutoka miaka sita hadi miaka minne.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top