
MSHAMBULIAJI wa
klabu ya Manchester City, Sergio
Aguero anaweza kufungiwa michezo
mitatu baada ya kumpiga kiwiko beki wa wagonga nyindo wa London, klabu ya West
Ham Winston Reid jana na kuwa na uwezekano wa kuukosa mchezo dhidi ya mahasimu
wao Manchester United.
Mchezaji huyo alimfanyia tukio hilo Reid kuelekea
mwishoni mwa mchezo huo ambao City walishinda 3-1, mabao yaliyofungwa na Raheem
Sterling (2) na Ferndandinho. Reid alitolewa mara moja baada ya tukio hilo na
kocha wake Slaven Bilic amsema alifanya hivyo kutokana na sababu za kiufundi.
Mwamuzi
wa mchezo huo Andre Marriner alikuwa karibu kabisa wakati tukio lile likitokea.
Aliamuru ipigwe free-kick na imeonekana kwamba hakujua kama Aguero alifanya
kitendo kile.
Lakini
pamoja na yote hayo FA wanaweza kuangalia upya video na kuitolea maamuzi.
Endapo
Aguero atakumbana na adhabu hiyo, basi anaweza kuukosa mchezo dhidi ya mahasimu
wao Manchester United utakaopigwa Old Trafford Septemba 10, mchezo mwingine
ukiwa dhidi ya Bournemouth kabla ya kumalizia na Swansea kwenye Kombe la EFL.
Meneja
wa Man City Pep Guardiola amesema: ‘Sikuliona tukio lile, hivyo siwezi kusema
chochote.’
‘Natumaini
hakuna baya litakalotokea. Na kama litatokea tutakubaliana nalo na kuendana
nalo. Kama tutampoteza basi ndiyo tumempoteza hivyo.’
Bosi
wa West Ham Slaven Bilic pia hakuona tukio hilo na kudai kwamba uamuzi wa
kumtoa Reid ulikuwa umezingatia zaidi sababu za kiufundi.
‘Sikumtoa
kwasababu ya tukio lile. Nilifanya vile kwasababu nilitaka kufanya madabiliko
tangu awali,’ Bilic alisema.
Post a Comment