
KLABU ya Manchester United imeanza vema kwenye mbio za ubingwa wa ligi kuu ya England, baada ya kuifunga timu ya AFC Bournamouth kwa jumla ya goli 3-1.
Klabu hiyo inayonolewa na Jose Mourinho, ilijipatia magoli yake kupitia kwa Juan Mata, 40, Wayne Rooney, 59 na Ibrahimovic, 64, huku goli la Bournamouth la kufutia machozi likifungwa na Adam Smith, 69.

United imecheza bila kumtumia mchezaji wao Ghali zaidi duniani, Paul Pogna amabae bado anatumikia kadi za njano za msimu uliopita kweny ligi kuu ya Italia.
Eric Baily ndiye aliyeibuka nyota wa mchezo kwa kuonyesha kiwngo bora kabisa kwnenye mchezo wake wa kwanza wa ligi kuu ya England.

Katika mchezo wa Arsenal VS Liverpool, wamefungana 1-1 ikiwa ni mapumziko mpaka sasa.

Post a Comment