
BAADA ya Mwenyekiti wa Yanga
Yusuf Manji kutangaza kujiuzulu nafasi ya mwenyekiti pamoja na kusitisha zoezi
lake la kuikodi klabu ya Yanga, Mashabiki na wanachama wa Yanga wamekusanyika
kwenye ofisi za klabu hiyo wakipinga kujiuzulu kwa Manji.
Baadhi ya wanachama na mashabiki wamekuwa
wakidai kwamba kuna watu ambao hawataki kumuunga mkono Manji katika zoezi zima
la kutaka kuikodi timu pamoja na nembo kwa miaka 10.
Aidha, moja ya watu ambao wamekuwa
wakitajwa kukwamisha zoezi hilo ni mzee Akilimali, pamoja na watu wengine wanaopinga
kusudi la mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji kuikodi klabu hiyo.
Manji amefikia
maamuzi hayo baada ya kusema kwamba amekuwa akitukanwa sana na baadhi ya watu
ambao hawataki Manji kuimiliki klabu hiyo ya Jangwani, “Hela za kwangu
mwenyewe, kwanini nikukanwe sasa? Basi waje wenjewe” Manji alisema.
Post a Comment