
LIGI kuu
ya England inaendelea tena leo kwa mchezo kati ya klabu ya Manchester United
dhidi ya watakatifu wa Southampton, mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Old
Trafford kuanzia majira ya saa nne za usiku kwa saa za Africa Mashariki.

Kwa
United ni mchezo wao wa pili wa EPL ambapo katika mchezo huo, kocha anatarajian
kuanzisha kikosi chake kamili ambacho Pogba pia atakuwepo baada ya kuukosa
mchezo wa awali kwa kadi ya njano.
Lakini
pia, Mourinho anatarajia kumwanzisha Chris Smalling baada ya mechi ya kwanza
kukaa nje kwa kadi ya njano uya msimu uliopita.
Kwa
upande wa Southampton, nahodha wao Jose Fonte, ambaye amekuwa akihusishwa na
mipnago ya kujiunga na United, anaweza kucheza licha ya kuukosa mchezo wa
ufunguzi kufuatia kuchelewa kujiunga na wenzake kwenye ‘pre-season’.
Ryan
Bertrand atakosekana kutokana na kusumbuliwa na majeraha na nafasi yake
itaendelea kuzibwa na Matt Targett.
Meneja
wa Southampton Claude Puel, amezungumzia juu ya tetesi za mchezaji wake Jose
Fonte kutakiwa na United:
”Sina
tatizo na Jose, ila ni suala la ajabu kidogo kuona tetesi hizi zinakuja wakati
tunakabiliana na mchezo dhidi ya United”
“Lakini
mbali na hayo ni mchezaji mzuri na amecheza vizuri mazoezini… Jose ana uzoefu,
hivyo hawezi kuchanganywa na masuala ya tetesi lakini kinachonishangazwa mimi
ni kuona tetesi hizi zinakuja kabla ya mchezo wetu, siku mbili kabla ya
mchezo.”
Japo
historia haina nafasi katika mpira wa miguu, kuelekea mchezo huo, hii ni
tathmini fupi zikutanapo timu hizi.
- Southampton wameibuka na ushindi wa bao 1-0 kwenye kila mchezo kati ya miwili iliyopita waliyocheza kwenye dimba la Old Trafford.
- Kabla ya hapo, ndani ya miaka 27 Southampton wamecheza michezo 19 ugenini dhidi ya United bila ya ushindi.
Post a Comment