![]() |
picha na salehe jembe. |
KAMATI ya sheria na hadhi za wachezaji
imelipitisha jina la mlinzi wa kulia wa Yanga Hassan Kessy Ramadhani kuitumikia
klabu hiyo baada ya hapo awali kuwepo na mvutano mkubwa na klabu yake ya zamani
Simba SC.
Simba
ilikuwa ikimtuhumu Kessy kuvunja mkataba kwa kuanza kuvaa jezi, kufanya
mazoezi, kusafiri na kushiriki shughuli mbalimbali za mabingwa hao wa VPL msimu
uliopita wakati muda wa mkataba wake na Wekundu hao wa Msimbazi haujafika
kikomo.
Kutokana
mgogoro huo, klabu ya Simba haikutoa barua (release letter) kumruhusu Kessy
kuitumikia Yanga ikidai kulipwa fidia na mchezaji huyo kwa kuvunja mkataba.
Sakata hilo lilimfanya Kessy kushindwa kujumuishwa kwenye kikosi cha Yanga
katika michuano ya kimataifa licha ya kuendelea kufanya mazoezi na kikosi cha
Hans van Pluijm.
Uamuzi
huo unamfanya Van Pluijm kuwa huru kumtumia Kessy kwenye mechi za ligi kuu
Tanzania bara kuanznia msimu mpya wa 2016/17 pamoja na ile michuano ya
kimataifa ambayo Yanga wataiwakilisha Tanzania kwenye klabu bingwa Afrika.
Kamati
ya sheria na hadhi za wachezaji awali ilikuwa ikutane Jumanne lakini
ilishindikana na baadae zikatoka taarifa kwamba, wachezaji wote walioombewa
leseni na vilabu vyao wataruhusiwa kucheza mchezo wa Ngao ya Jamii uliochezwa
Jumatano kati ya Yanga na Azam huku Kessy aliitumikia Yanga.
Leo
Ijumaa August 19 taarifa zimetoka kwamba Kessy yuko huru kuitumikia Yanga baada
ya kamati hiyo kukaa na kupitia kesi zote za usajili ikiwemo ya Kessy.
Aidha,
baada ya charleskunji.blogspot.com kufanya mahojiano na msemaji wa TFF juu ya
shtaka la klabu ya Simba ya Kessy kucheza mechi ya ngao ya jamii, Lucas
amelitupilia mbali na kusema kwamba Kessy aliruhusiwa kucheza mchezo huo.
Post a Comment