
KIUNGO mshambuliaji wa klabu ya
mashetani wekundu, Bastian Schweinsteiger amesema kwamba bado ana furaha kuishi
jijini Manchester licha ya kutojumuishwa kwenye kikosi cha timu hiyo na kocha
Jose Mourinho.
Mjerumani huyo ameondolewa na kuwekwa
kwenye kikosi cha akiba na kocha Jose Mourinho, ambaye alithibitisha kwamba
haihitaji tena huduma ya Schweinsteiger.
Schweinsteiger anatarajiwa
kuondoka United mwishoni mwa dirisha hili la usajili na ametoa upadate nyingine
kwa mashabiki wake kupitia ukurasa wake wa Twitter ametweet:
“Baada ya mizunguko yangu,
nafurahia muda uliosalia katika siku ya leo hapa Manchester. Natumaini wote mna
siku njema!”
United wanaonekana hawana
mpango tena na Schweinsteiger na kaka yake Bastian, Tobi Schweinsteiger
alinukuliwa akikosoa kitendo hicho alichofanyiwa mdogo wake na ku-tweet: “No
respect.”
Mpaka sasa, United wanaviungo wa kati
watano ambao ni Paul Pogba, Michael Carrick, Morgan Schneiderlin, Marouane
Fellaini na Ander Herrera.
Ripoti zinaeleza kwamba, klabu za AC na
Inter Milan zinahitaji huduma ya Schweinsteiger, ambaye atatakiwa kupunguza
sana mshahara wake endapo ataamua kuondoka.
Anatajwa kupokea kiasi cha paundi 200,000
kwa wiki.
Msimu uliopita, Schweinsteiger alianza
kwenye michezo 21 na michezo 10 aliingia kutokea benchi.
Post a Comment