SPORTS

 

Unknown Unknown Author
Title: AZAM FC IMETWAA NGAO YA JAMII KWA KUIFUNGA YANGA.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
KLABU ya Azam imeibuka kidedea kwa kuichapa jumla ya penalty 4-1 katika mchezo wa ngao ya jamii wa kuukaribisha msimu mpya wa ligi wa 2...
IMG_0401

KLABU ya Azam imeibuka kidedea kwa kuichapa jumla ya penalty 4-1 katika mchezo wa ngao ya jamii wa kuukaribisha msimu mpya wa ligi wa 2016-2017 baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya goli 2-2.
Yanga ambao walikuwa wakiishikilia Ngao ya Jamii baada ya kuifunga Azam kwenye mchezo wa msimu uliopita kwa changamoto ya mikwaju ya penati, walikuwa kwenye nafasi nzuri ya kubeba tena ngao hiyo kutokana na kuongoza mchezo huo kwa magoli 2-0, magoli yaliyofungwa kipindi cha kwanza.
Mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma alifunga bao la kwanza dakika ya 20 kwa njia ya penati kufuatia yeye mwenyewe (Ngoma) kuanngushwa kwenye box na beki wa Azam David Mwantika.
Dakika moja baadaye, Ngoma akaifungia tena Yanga bao la pili akiunganisha pasi ya Amis Tambwe ambaye alitumia vizuri makosa ya Mwantika aliyeshindwa ku-control mpira na kunyang’anywa na Tambwe.
IMG_0279


Dakika 45 za kipindi cha kwanza zikamalizika kwa Yanga kuwa mbele kwa mabao 2-0 dhidi ya Azam FC.
Dakika ya 74 Shomari Kapombe aliipatia Azam bao la kwanza akitumia makosa ya mabeki wa Yanga waliozembea kuondosha mpira kwenye eneo la hatari la goli lao.
John Bocco ‘Adebayor’ aliisawazishia Azam kwa mkwaju wa penati dakika ya 90 penati iliyotokana na beki wa Yanga kuushika mpira kwenye box

IMG_0323

Deogratius Munishi ndiye mchezaji pekee aliyefunga penati kwa upande wa Yanga huku Hassan Kessy akishuhudia penati yake ikidakwa na golikipa wa Azam Aishi Manula wakati Haruna Niyonzima yeye penati yake iligonga ‘mtambaa panya’ na kutoka nje.

Katika kipindi cha miaka mitano ya hivi karibuni, Azam na Yanga zimekutana mara nne mfululizo kuwania Ngao ya Jamii huku Yanga wakiongoza kuinyakua mara nyingi zaidi ya wapinzani wao.
Yanga wametwaa ngao hiyo mara tatu (mara zote kwa kuifunga Azam) huku ushindi wa leo ukiwapa Azam ngao hiyo kwa mara ya pili.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top