
Klabu ya Watford ya nchini Wingereza imemsajili beki wa kati
wa klabu ya Napoli Juan Camilo Zuniga
kwa mkopo lakini
akitarajiwa kuongeza mkataba akifanya vyema.
Zuniga atakayeichezea Watford kwa msimu ujao wakati
akitarajiwa ku extend mkataba endapo viongozi wa klabu hiyo kama watavutiwa na
huduma yake.
Zuniga anajiunga na aliyekuwa kocha wa zamani wa Napoli msimu
wa 2009-2013, aliyesini kuifundisha klabu ya Watford Walter Mazzari.
Zuniga amecheza mechi 62 katika timu ya taifa ya Colombia na
alifanikiwa kucheza mara nne katika fainali za kombe la dunia zilizofanyika
huko nchini brazil mwaka 2014 na kuwashuhudia timu ya taifa ya Ujerumani kutwaa
kombe hilo kwa kuwafunga timu ya Argentina kwa goli moja kwa sifuri.
Zuniga, raia wa Colombia, anaweza kucheza upande wa kulia na
kushoto na aliweza kujiunga na Bologna kwa mkopo baada ya kupoteza namba katika
kikosi cha Napoli lakini pia kuweza kujiunga na Watford kwa mkopo.
Zuniga 30, anakuwa mtu wan ne kutia kandarasi klabuni hapo
huku Mazzari akiwa anaendelea kuhakikisha anatengeneza kikosi bora cha kuweza
kupambana ili kuhakikisha wanafanya vyema.
Post a Comment